Mtoto awakilisha mashabiki nchi nzima

Mtoto wa miaka mitano Bernadetha Joseph Mwamboneke amewawakilisha mashabiki wetu nchi nzima katika hafla ya kuwashukuru kwa kuwa pamoja nasi msimu mzima wa 2021/22.

Uongozi wa klabu umetumia mchezo wetu wa mwisho wa nyumbani tuliocheza na Mtibwa Sugar kuwashukuru mashabiki kwa mchango wao mkubwa waliotupa tangu mwanzo mpaka leo.

Mtendaji Mkuu wa Klabu, Barbara Gonzalez amemkabidhi mtoto Bernadetha jezi maalumu ikiwa na maana ya kuwashukuru mashabiki wote nchi nzima.

Kabla ya kumkabidhi Bernadetha jezi hiyo, Barbara alitembelea vikundi vyote vya hamasa vilivyojitokeza uwanjani kwenda kuwashukuru.

Baada ya kumalizika kwa mchezo Viongozi na Maafisa wa klabu walishuka chini ya uwanja na kuwapungia mashabiki kuonyesha tunawathamini.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER