Mashabiki wamwagia pesa Wawa wakimuaga

Mashabiki waliojitokeza katika Uwanja wa Benjamin Mkapa wamemwagia pesa mlinzi wa kimataifa, Pascal Wawa wakati wa kuagwa baada ya kumalizika mchezo wetu dhidi ya Mtibwa Sugar.

Mchezo wa leo ni wa mwisho kwa Wawa kucheza ndani ya kikosi chetu baada ya kudumu kwa miaka mitano na ulipangwa rasmi kumuaga nyota huyo wa kimataifa kutoka Ivory Coast.

Mashabiki wetu wameonyesha upendo mkubwa kwa Wawa kama ilivyokuwa kwa kiungo mshambuliaji Rally Bwalya ambaye naye alitunzwa pesa.

Tumeweka utaratibu mzuri kwa kuhakikisha tunamalizana vizuri na wachezaji wetu kwa kuwaaga mbele ya mashabiki wetu kutokana na kuthamini michango yao ndani ya klabu yetu.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER