Kikosi kitakachotuwakilisha dhidi ya Vipers Leo

Leo saa moja usiku kikosi chetu kitashuka katika Uwanja wa St. Mary’s uliopo Entebe, Uganda kuikabili Vipers katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya makundi.

Kocha Mkuu Roberto Oliviera ‘Robertinho’ amefanya mabadiliko ya wachezaji watatu ukilinganisha na kikosi kilichoanza katika mchezo wetu wa mwisho wa ligi dhidi ya Azam FC.

Moses Phiri ataongoza safu ya ushambuliaji akichukua nafasi ya nahodha John Bocco, Kibu Denis akichukua nafasi ya Pape Sakho wakati Joash Onyango akirejea kwenye nafasi yake huku Kennedy Juma akianzia benchi.

Kikosi kamili kilivyopangwa:

Aishi Manula (28), Shomari Kapombe (12), Mohamed Hussein (15), Joash Onyango (16), Henock Inonga (29), Sadio Kanoute (13), Kibu Denis (38), Mzamiru Yassin (19),  Moses Phiri (25), Saido Ntibazonkiza (39), Clatous Chama (17).

Wachezaji wa Akiba

Beno Kakolanya (30), Israel Patrick (5), Kennedy Juma (5), Erasto Nyoni (18), Pape Sakho (10), Peter Banda (11), John Bocco (22), Jean Baleke (4), Habibu Kyombo (32)

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER