Kikosi kitakachotuwakilisha dhidi ya RS Berkane leo

Kocha Mkuu Pablo Franco, leo atawaanzisha viungo watatu wakabaji katika mchezo wetu wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya RS Berkane utakaopigiwa saa nne usiku kwa saa za nyumbani.

Henock Inonga amepangwa kiungo wa ulinzi sambamba na Erasto Nyoni pamoja na Sadio Kanoute huku Joash Onyango na Kennedy Juma wakisimama kama walinzi wa kati

Nahodha John Bocco ataongoza mashambulizi wakati Peter Banda na Pape Ousmane Sakho wakishambulia kutoka pembeni.

Kikosi Kamili kilivyopangwa

Aishi Manula (28), Shomari Kapombe (12), Mohamed Hussein (15), Joash Onyango (16), Kennedy Juma (26), Henock Inonga (29), Peter Banda (11), Erasto Nyoni (18), John Bocco (22), Sadio Kanoute (13), Pape Sakho (17)

Wachezaji wa akiba

Beno Kakolanya (30), Ally Salim (1), Israel Patrick (5), Gadiel Michael (2), Bernard Morrison (3), Medie Kagere (14), Yusuf Mhilu (27) Jimmyson Mwinuke (21).

SHARE :
Facebook
Twitter

One Response

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER