Kauli ya Matola kuelekea mchezo wa Kesho

Kaimu Kocha Mkuu Seleman Matola, amesema maandalizi yamekamilika kuelekea mchezo wa kesho wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Mbeya City utakaopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa saa moja usiku.

Matola amesema kikosi kimefanya mazoezi kwa wiki mbili na kimekamilika baada ya wale waliokuwa kwenye majukumu ya timu za taifa kujiunga pamoja na wenzao.

Matola ameweka wazi kuwa sisi ni timu kubwa na tunahitaji kushinda kila mchezo uliopo mbele yetu ikiwemo wa kesho bila kujali tunapambania ubingwa au la.

“Tuko tayari kwa mchezo wa kesho mchezo wa kesho, wachezaji wapo kwenye hali nzuri maandalizi yamekamilika na tuna imani tutapata alama zote tatu.

“Tunaiheshimu Mbeya City, inatupa ushindani mkubwa tukikutana nayo lakini tupo tayari kukabiliana nao kulingana na maandalizi tuliyofanya,” amesema Matola.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER