Kalaba kuiongoza TP Mazembe Simba Day

Kiungo wa Timu Taifa ya Zambia, Rainford Kalaba anatarajiwa kuwa sehemu ya wachezaji 23 wa TP Mazembe watakaokuja nchini Septemba 18 kwa ajili ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Simba katika Tamasha la Simba Day Septemba 19, mwaka huu katika Uwanja Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Nyota huyo ambaye ni miongoni mwa wachezaji wakongwe wa timu hiyo atakuwa sehemu ya msafara huo ambao pia utakuwa na viongozi 12 na kufanya msafara huo kuwa na watu 35.

Simba imekuwa na mahusiano mazuri na timu hiyo kutoka Congo na mara kadhaa imekuwa ikicheza nayo michezo ya kirafiki. Mara ya mwisho kikosi hicho kuja nchini ni mwanzoni mwa mwaka huu ambapo ilikuja kushiriki mashindano ya Super Cup yaliyoandaliwa na Simba.

Kikosi Kamili

1.            Mounkoro Ibrahim

2.            Said Ngusia Baggio

3.            Ochaya Joseph Benson

4.            Atibu Radjabu Johnson

5.            Issama Mpeko Djos

6.            Masengo Yumba Godet

7.            Tandi Mwape

8.            Luzolo Nsita Ernest

9.            Mundeko Zatu Kelvin

10.          Kouame Koffi Cristian Raoul

11.          Zemanga Soze Soze

12.          Kalaba Rainford

13.          Mayombo Etienne Raby

14.          Sudi Bibonge Gondry

15.          Mika Michee Michee

16.          Bossu Nzali Adam

17.          Kinzumbi Phillippes Beni

18.          Ngimbi Vumbi Merceil

19.          Bileko Mbaki Kelvin

20.          Baleke Othos Jean

21.          Beya Tumuteka Joel

22.          Ntambwe Kalonji Magloire

23.          Zola Kiaku Arsene

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER