Ije mvua, lije jua hatoki mtu Majimaji leo

Kikosi chetu leo kinashuka dimbani kucheza mechi ya nusu fainali ya Michuano ya Azam Sports Federation Cup (ASFC) dhidi ya Azam FC utakaopigwa Uwanja wa Majimaji hapa Songea saa tisa alasiri.

Benchi la ufundi, wachezaji, viongozi na mashabiki wetu wanaamini utakuwa mchezo mgumu kutokana na ubora wa wapinzani lakini hata hivyo tuna matumaini makubwa ya kuibuka na ushindi.

Kocha Mkuu, Didier Gomes ameweka wazi kuwa malengo yetu msimu huu yalikuwa kutwaa mataji yote ya ndani hivyo tutapigana kwa kila njia kuhakikisha tunafanikisha.

“Tangu mwanzo wa msimu lengo letu lilikuwa ni kutetea taji hili na tumefika hatua hii kwa hiyo tumejipanga kushinda na kuingia fainali.

“Azam ni timu nzuri na tunakumbuka mchezo wa mwisho tulipokutana nao tuliweza kumiliki mchezo ila tulipoteza nafasi nyingi hasa kipindi cha kwanza lakini tumejitahidi kuondoa mapungufu kama hayo ili kupata ushindi leo,” amesema Kocha Gomes.

Kwa upande wake Nahodha, John Bocco amesema wachezaji wote wana ari na kila mmoja atakayepewa nafasi ya kucheza yupo tayari kuipigania timu.

NI MECHI YA KISASI

Tulipokutana katika mchezo wa mwisho ligi kuu mzunguko wa kwanza uliofanyika Uwanja wa Benjamin Mkapa, Februari 7, mwaka huu tulitoka sare ya mabao 2-2 hivyo kila timu itataka kushinda ili kuonekana mbabe na ndiyo kisasi chenyewe.

SAFARI YETU HADI KUFIKIA LEO

HATUA YA 64 BORA

Simba 5-0 Majimaji

HATUA YA 32 BORA

African Lyon 0-3 Simba

HATUA YA 16 BORA

Simba 2-1 Kagera Sugar

HATUA YA ROBO FAINALI

Simba 3-0 Dodoma Jiji

Mshindi wa mchezo wa leo atakutana na Yanga katika mchezo wa fainali utakaopigwa Julai 25 mwaka huu kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma.

SHARE :
Facebook
Twitter

One Response

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER