Hivi hapa viingilio vya mchezo wetu dhidi ya Raja Casablanca

Kiingilio cha chini ya mchezo wetu wa pili wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Raja Casablanca utakaopigwa Uwanja wa Benjamin Mkapa, Februari 18 kitakuwa Sh. 5000.

Viingilio vimetangazwa mapema ili kuwapa nafasi mashabiki kununua mapema sababu tunahitaji mashabiki wajitokeze kwa wingi uwanjani kuipa sapoti timu.

Viingilio ni kama ifuatavyo:

Mzunguko Sh. 5000
VIP B & C Sh. 20000
VIP A Sh. 30,000
Platinum Sh. 100,000
Platinum Plus Sh. 150,000

Vitu ambavyo atavipata atayenunua tiketi za Platinum ni.

1. Escort kutoka Hoteli ya Hyatt Regency mpaka uwanjani.

2. Kifurushi maalum kutoka Simba.

3. Chakula na Vinywaji ukiwa uwanjani.

Ili kupata tiketi za Platnum na Platnum Plus tupigie kwa namba hii +255742771311.

Tayari tiketi zimeanza kuuzwa kwa njia ya mtandao muda mfupi ujao tutatangaza vituo ambavyo zitapatikana.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER