Gomez awabadilishia gia angani Mwadui, Luis aanzia benchi Chikwende ndani

Kocha Mkuu, Didier Gomez amefanya mabadiliko kidogo kwenye kikosi cha kwanza kuelekea mchezo wa leo wa Ligi Kuu dhidi ya Mwadui FC utakaofanyika Uwanja wa CCM Kambarage Shinyanga.

Gomez amemuanzisha benchi kiungo mshambuliaji Luis Miquissone ambaye amekuwa akianza katika kila mchezo kutokana ubora alionao huku Perfect Chikwende akichukua nafasi yake.

Kocha huyo leo amempunzisha kiungo Taddeo Lwanga ambapo eneo la kiungo wa ulinzi litakuwa chini ya Erasto Nyoni na Jonas Mkude.

Kikosi Kamili kilivyopangwa

1. Aishi Manula

2. Shomari Kapombe

3. Mohamed Hussein ©

4. Joash Onyango

5. Pascal Wawa

6. Erasto Nyoni

7. Clatous Chama

8. Jonas Mkude

9. Medie Kagere

10. Rally Bwalya

11. Perfect Chikwende

Wachezaji wa Akiba

GK. Beno Kakolanya

02. Kennedy Juma

03. Mzamiru Yassin

04. Bernard Morrison

05. Chris Mugalu

06. John Bocco

07. Luis Miquissone

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER