Chama mchezaji bora mwezi Aprili

Kiungo mshambuliaji, Clatous Chama amechaguliwa mchezaji bora wa mashabiki wa mwezi wa Aprili (Emirate Aluminium Simba Fans Player of the Month).

Chama raia wa Zambia amewashinda mlinda mlango Aishi Manula na mlinzi wa kulia Shomari Kapombe ambao aliingia nao fainali.

Tuzo hii inadhaminiwa na Emirate Aluminium Profile hushindanisha nyota watano waliofanya vizuri zaidi kabla ya kuchujwa hadi watatu na Kamati maalumu na kupigiwa kura na mashabiki hadi mshindi apatikane.

Chama anakuwa mchezaji wa tatu kuchukua tuzo hiyo tangu ilipoanza kutolewa Februari baada ya Luis Miquissone na Joash Onyango.

Huu hapa mchanganuo wa kura zilivyopigwa:

Clatous Chama – 50.48%

Aishi Manula – 30.74%

Shomari Kapombe – 18.78%

SHARE :
Facebook
Twitter

9 Responses

  1. Hello! I could have sworn I’ve visited this web site before but
    after going through a few of the posts I realized it’s new to me.

    Anyways, I’m definitely delighted I came across it and I’ll be bookmarking it and checking back regularly!

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER