Mwanachama mwandamizi na mdhamini wazamani wa Klabu, Mzee Azim Dewji amewaomba wapenzi na mashabiki wetu kujitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Benjamin Mkapa kwa ajili ya kuisapoti timu kuelekea mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Al Masry utakaopigwa Jumatano Uwanja wa Benjamin Mkapa.
Mzee Azim amesema anaamini wingi wa mashabiki ambao watajitokeza katika Uwanja wa Benjamin Mkapa utakuwa chachu ya ushindi kwa asilimia 50 kabla ya timu kushuka dimbani.
Tazama video hii hadi mwisho Mzee Azim amefunguka mengi kuhusu mchezo dhidi ya Al Masry.