Daktari wa timu, Edwin Kagabo amesema wachezaji wote waliokuwa majeruhi wamerejea kikosini na wapo tayari kwa ajili ya mechi zilizopo mbele yetu.
Mlinda mlango Moussa Camara, walinzi Valentine Nouma na Che Fondoh Malone pamoja na kiungo Mzamiru Yassin ambao walikuwa majeruhi wamerejea na wanafanya mazoezi pamoja na wenzao.
Tazama mahojiano haya hadi mwisho Dkt. Kagabo amezungumzia hali halisi ya kikosi mpaka sasa.