Tumepangwa na Al Masry Robo Fainali Shirikisho

Droo ya hatua ya robo fainali imekamilika Doha, Qatar na tumepangwa kucheza na Al Masry kutoka Misri.

Tutaanzia ugenini mchezo wa kwanza utapigwa kati ya Aprili 1-2 huku mechi ya marudiano ikipigwa kati ya Aprili 8-9.

Tumewahi kukutana na Al Masry kwenye michuano hii ambapo tulipokutana mwaka 2018.

Katika mchezo wa mkondo wa kwanza tukiwa nyumbani tulitoka sare ya mabao 2-2 na mechi ya marudiano nchini Misri ikamalizika kwa sare ya bila kufungana.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER