Timu kuondoka Ijumaa kuifuata ASEC Benin

Kikosi chetu kitaondoka Ijumaa alfajiri kuelekea nchini Benin kwa ajili ya mchezo wetu wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya ASEC Mimosas utakaopigwa Jumapili saa moja jioni.

Mchezo huo utafanyika Benin badala ya Ivory Coast ambapo ni nyumbani kwa ASEC kutokana na viwanja vyao kuwa kwenye ukarabati mkubwa ikijiandaa na michuano ijayo ya AFCON.

Kikosi kitaondoka saa tisa alfajiri na Ethiopia Airline kikiwa na wachezaji 24, benchi la ufundi na viongozi.

Tutaingia katika mchezo huo tukiwa na lengo la kutafuta alama tatu muhimu ili kujihakikishia nafasi ya kuingia robo fainali ya michuano hiyo.

SHARE :
Facebook
Twitter

One Response

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER