Timu kuifuata Kagera leo mchana

Kikosi chetu kitaondoka mchana kuelekea mkoani Kagera kwa ajili ya mchezo wetu ujao wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Kagera Sugar.

Mchezo huo utapigwa katika Uwanja wa Kaitaba Jumamosi, Desemba 18 saa 10 jioni ambapo tumejipanga kupata alama tatu muhimu.

Baada ya mchezo wa juzi wa Azam Sports Federation Cup dhidi ya JKT Tanzania wachezaji walipewa mapumziko ya siku moja kabla ya kuanza safari kuelekea Kagera.

Kikosi kizima kitasafiri ili kulipa nafasi benchi la ufundi kuchagua nani aanze lengo likiwa ni kupambana kuhakikisha tunarudi na alama zote tatu jijini Dar es Salaam.

SHARE :
Facebook
Twitter

One Response

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER