Queens yawaacha nyota 11

Katika kufanya mabadiliko makubwa ya kikosi kuelekea msimu mpya wa mashindano 2025/2026 timu yetu ya Simba Queens imewaacha wachezaji 11.

Mabadiliko hayo yanatokana na malengo tuliyojiwekea kuelekea msimu ujao hasa ukizingatia msimu uliopita tulishindwa kutetea ubingwa wetu.

Nyota hao wengi wao mikataba yao imemalizika huku wachache wakiondoka kutokana na makubaliano ya pande mbili.

Wachezaji hao ni Ritticia Nabbosa, Precious Christopher, Wincate  Kaari, Asha Djafari na Gelwa Yonah.

Wengine ni Josephine  Julius, Asha Rashid, Mary Saiki, Carolyene Rufa, Jackline Albert  na Daniella Ngoyi.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER