Bao pekee lililofungwa na Steven Mukwala limetosha kutupa alama tatu mbele ya Singida Black Stars katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa Uwanja wa KMC Complex.
Tulianza mchezo huo kwa kasi huku tulitengeneza nafasi nyingi za kufunga lakini hata hivyo tulikosa umakini wakuzitumia.
Mukwala alitupatia bao hilo pekee dakika ya 42 baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Jean Charles Ahoua na kuwazidi ujanja walinzi wa Singida.
Dakika 15 za mwanzo za kipindi cha pili Singida walifika mara kadha langoni kwetu lakini safu yetu ya ulinzi ilikuwa imara kuondoa hatari zote.
Ushindi huu umetufanya kufikisha pointi 72 baada ya kucheza mechi 27 tukiendelea kusalia nafasi ya pili alama moja nyuma ya vinara.
X1: Camara, Kapombe, Zimbwe Jr, Chamou, Che Malone, Kagoma, Mutale (Kibu 67′) Ngoma, Mukwala (Ateba 83′), Ahoua (Fernandez 82′), Mpanzu (Hamza 60′)
Waliionyeshwa kadi: Camara 82′
X1: Obasogie, Koffi (Rupia 81′), Imoro (Kennedy 81′), Tra Bi, Assinki, Nashon (Damaro 45′), Chukwu, Bada, Adebayor (Keyekeh 67′), Tchakei (Pokou 45′), Sowah
Waliionyeshwa kadi: Nashon 29′ Damaro 73′ Sowah 90+4′