Bao la kiungo mshambuliaji Pape Sakho alilofunga dhidi ya ASEC Mimosas katika mchezo wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika limechaguliwa kuingia 10 bora barani Afrika likishindania bao bora la mwaka.
Sakho alifunga bao hilo kwa ‘acrobatic’ akimalizia mpira wa krosi uliopigwa na Shomari Kapombe kutoka upande wa kulia.
Mchezo huo umbao ulikuwa mkali na wakupendeza ulipigwa Februari 13 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.