Tuzo yamuongezea mzuka Kibu

Kiungo mshambuliaji Kibu Denis, amesema tuzo ya mchezaji bora wa mashabiki mwezi Mei (Emirate Aluminium ACP Simba Fans Player of the Month) imemuongezea morali ya kuendelea kujituma kuisaidia timu.

Kibu amesema kila mchezaji anafanya jitihada kubwa kufanya vizuri uwanjani kuisaidia timu na kupata tuzo kunaongeza thamani yake.

Pamoja na mambo mengine pia amewashukuru mashabiki waliompigia kura, wachezaji waliompa ushirikiano uwanjani pamoja na benchi la ufundi kwa kumpa nafasi huku akiahidi makubwa zaidi.

“Ni furaha kwangu kama mchezaji kupata tuzo hii. Nawashukuru mashabiki kwa kunipigia kura, wachezaji wenzangu na benchi la ufundi kwa ushirikiano. Hii itakuwa chachu kwangu kuendelea kuipigania timu,” amesema Kibu.

Kwa upande wake Ofisa Mahusiano wa Emirate Aluminium ACP, Issa Maeda amempongeza Kibu kwa kufanya vizuri mwezi Mei na kufanikiwa kuchukua tuzo hiyo baada ya kuibuka mshindi.

Maeda amewaomba wateja waendelee kununua bidhaa za Emirate Aluminium hasa mpya iliyoingia karibuni ya European Style.

“Tumekuja na bidhaa mpya inayojulikana kama European Style au Slide ambayo ni chuma kipya kwa ajili ya kupendezesha nyumba ambacho ni imara chenye muonekano mzuri. Wateja wetu tunaomba muendelee kununua bidhaa zetu ambazo zinaboresha mara kwa mara,” amesema Maeda.

Katika mwezi Mei, Kibu amecheza mechi saba sawa na dakika 630 akifunga mabao matano na kusaidia kupatikana kwa bao moja.

SHARE :
Facebook
Twitter

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

GET NEWSLETTER