Mlinda mlango, Moussa Camara ameifikia rekodi ya Aishi Manula ya kutoruhusu bao (Clean sheet) 19 katika mechi za Ligi Kuu msimu huu.
Manula alifanya hivyo msimu wa 2017/18 baada ya kucheza mechi 30 na kufanikiwa kuwa mlinda mlango bora wa Ligi huku tukitwaa ubingwa wa ligi.
Tayari Camara ameifikia rekodi hiyo lakini akiwa amecheza mechi 27 sawa na dakika 2430.
Huu ni msimu wa kwanza wa Camara kucheza Ligi Kuu ya NBC Tanzania na ameonyesha kiwango bora na amekuwa na mchango mkubwa uwanjani akichangia mafanikio tuliyopata.
Tumemsajili Camara kutoka Horoya FC ya Guinea mwanzoni mwa msimu na amekuwa muhimili mkubwa kwenye lango letu.